Siku ya Wanawake Watetezi

Maadhimisho ya Siku wa Wanawake watetezi Duniani

Mtandao wa Wanawake Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (CWHRDs Tanzania) umeadhimisha siku ya wanawake watetezi wa haki za binadamu duniani katika ukumbi wa hotel ya Sleepway jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Dr John Jingu katibu mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto. Maadhimisho hayo hufanyika kila tarehe 29/11 kuwakumbuka na kuwapa heshima wanawake wote watetezi wa haki za binadamu ambapo Mtandao uliwatunuku cheti wanawake vinara watetezi wa haki za binadamu. Waliotunukiwa vyeti ni pamoja na...

  • Geline Fuko, Mkurugenzi wa Shirika la TANGIBLE Tanzania ametunukiwa kama mwanamke kinara mtetezi katika nyanja ya democrasia na utawala bora
  • Francisca Damian, Mkurugenzi wa shirika la Ladies Joint Forum ametunukiwa kama kinara wa kuwawezesha wanawake kiumichumi
  • Sophia Donald, Mkurugenzi wa Shirika la Sauti ya Wanawake Ukerewe ametunukiwa kama kinara wa utetezi wa haki ya afya ya uzazi na mabinti
  • Esta Pamagila, mwanaharakati wa kujitegemea, ametunukiwa kama mwanamke kinara mtetezi wa kukomesha ukatili wa kijinsia kwa wanawake na wasichana waiishio vijijini
  • Rose Serwatt, Mkurugenzi wa shirika la Tanzania Widows Association (TAWIA) alitunukiwa kama mwanamke mtetezi kinara wa kuwatetea wanawake wajane
  • Gema Akilimali, Mwenyekiti wa TGNP, ametunukiwa kama nguli wa kutetea haki za wanawake Tanzania

Katika maadhimisho hayo kulikuwa na mdahalo wa Unyanyasaji wa Kingono Mahali pa kazi ulioongozwa na Jackiline Tung'ombe wa shirika la PGWOCADE, huku wazungumzaji wakiwa ni Mery Rusimbi mkurugenzi wa shirika la Women Fund Truste Tanzania, Anna Kulaya Mkuregenzi wa WiLDAF, na Nabor Assey kutoka ofisi ya Tume ya Hakiza Binadamu na Utawala Bora Tanzania.


Pia kulikuwa na mdahalo wa mauaji ya wanawake na wapenzi ulioongozwa na Getrude Dyabane wa kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Tanzania (LHRC), wazungumzaji wakiwa ni Lulu Urio Mkurugenzi wa Shirika la Hodari, Wakili Anna Henga Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Tanzania, pamoja na Dr Evaristo Longopa kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu Tanzania.


Mdahalo mwingine ulikuwa ni Ukatili wa Kijinsia Mtandaoni pamoja na Udhalilishaji wa Wanawake na Wasichana. Mdahalo huu uliongozwa na Marcela Lungu Mkurugenzi wa TIBA Tanzania huku wachangiaji wakiwa ni Zaituni Njovu Mkurugenzi wa Zaina Foundation, Asteria katunzi kutoka shirika la TGNP.

Members

66

Members Registered

Litigation

2

Cases Intervened

Projects

2

Projects Completed

Copyright © CWHRDs-Tanzania